MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU WETU NA VITU VYOTE VILIVYO HAL
"Katika mwanzo Mungu aliumba mbigu na dunia." Mwanzo 1:1
"Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa vilivyo mbinguni na vilivyo duniani...." Wakolosayi 1:16
"Mubarikwe ninyi na BWANA, aliyefanya mbigu na dunia. Mbingu ni mbingu za BWANA, lakini amewapa wana wa watu inchi." Zaburi 115:15, 16
MUNGU ALITUUMBA
"Mungu akasema: Tufanye mutu kwa mufano wetu, mwenye sura yetu, na watawale...juu ya inchi nzima ....'" Mwanzo 1:26
MUTU ALIKUWA NAFSI YA UHAI
"BWANA Mungu akafanya mutu wa mavumbi ya inchi, akapuliza pumuzi ya uzima ndani ya pua yake; na mutu alikuwa nafsi* ya uhai." Mwanzo 2:7
"BWANA Mungu akasema: Si vema mutu awe peke yake; nitamufanyia musaidia....Na BWANA Mungu alileta usingizi muzito kuangukia mutu, akalala; akatwaa mumoja wa mifupa ya mbavu zake, akafunga nyama kwa pahali penyewe; na mufupa wa mbavu BWANA Mungu alioondosha kwa mutu, akafanya mwanamuke, akamupeleka karibu na mutu.'' Mwanzo 2:18, 21-22
*Nafsi hai maana yake tutakuwa pahali fulani milele.
ADAMU NA HAWA WALIASI MUNGU
Hatungesikiliza
Kamwe sauti ya Shetani.
"BWANA Mungu akatwaa mutu, akamutia shambani mwa Edeni kulilima na kulichunga. BWANA Mungu akaagiza mutu akisema: wa kila muti wa shamba unaweza kula; lakini wa muti wa kujua uzuri na ubaya usile kwa maana siku unapokula, hakika utakufa." Mwanzo 2:15-17
NYOKA ALIYEITWA VILE DIABOLO AO SHETANI ALIPUUZI MAMLAKA YA MUNGU NAYE AKASEMA UWONGO.
"Nyoka akamwambia mwanamuke: Hakika hamutakufa. Na wakati mwanamuke alipoona ya kama muti ulikuwa muzuri kwa chakula, na ya kama ulipendeza macho, na ya kama ulikuwa muti wa kutamaaniwa akatwaa...akakula; akamupa mume wake vilevile...naye alikula." Mwanzo 3:4, 6
ADAMU NA HAWA HAWAKUWEZA TENA KUKAA KATIKA SHAMBA
"...BWANA
Mungu akamutoa toka shamba la Edeni, alime udongo pale
alipotwaliwa....akaweka makerubi...na upanga wa ulimi wa
moto...kuchunga nija ya muti wa uzima." Mwanzo 3:23, 24
ILIKUWA SIKU YA HUZUNI KWA WANADAMU WAKATI ADAMU NA HAWA WALIFANYA ZAMBI
"...Kwa mutu mumoja zambi iliingia ulimwenguni, na kufa kwa nija ya zambi; na hivi kufa kulikuja juu ya watu wote...." Waroma 5:12
MUPANGO WA MUNGU KUTUOKOA TOKA ZAMBI ULIKUWA KUTUMA MWANA WAKE WA PEKEE
"Naye
atazaa Mwana; nawe utamwita jina lake Yesu, kwa sababu ndiye
atakayeokoa watu wake toka zambi zao." Matayo 1:21
Kwa kukaribia wanadamu, Mwana wa Mungu alipashwa kuja kama Mwana wa mutu. "Maana katika yeye (Yesu Kristo) unakaa utimilifu wote wa Mungu kwa mwili.'' Wakolosayi 2:9
YESU KRISTO ZABIHU YETU TAKATIFU
Yesu ni Mwana-kondoo wa Mungu. "Tazama Mwana- Kondoo wa Mungu anayechukua zambi ya ulimwengu." Yoane 1:29b
"...Tumepata utakaso (tumefanywa takatifu) kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja." Waebrania 10:10
"...Tukihesabiwa haki (Tumehesabiwa vema) sasa kwa damu yake, tutaokolewa katika gazabu kwa yeye."Waroma 5:9
"...Wakati tulipokuwa tungali wenye zambi [kutotii Mungu],
Kristo alikufa kwa ajili yetu." Waroma 5:8
WOTE WANAOAMINI MWANA WA MUNGU WANA UZIMA
"Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee, ili kila mutu akimwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele." Yoane 3:16
"AMEFUFUKA!"
"Malaika
akajibu, akawaambia wanawake: Mu-
siogope; kwa sababu ninajua ya kama munatafuta Yesu aliyesulibiwa. Yeye si hapa; kwani amefufuka kama alivyosema. Kujeni mwone pahali Bwana alipolala." Matayo 28:5, 6
YESU ANAWEZA KUKUOKOA NAYE ANAKUOMBEA
"Lakini yeye, kwa sababu anakaa hata milele...anaweza kuokoa kabisa wao wanaokuja kwake Mungu kwa njia yake; maana yeye ni hai siku zote apate kuwaombea (kuwatetea)." Waebrania 7:24, 25
YESU NI NJIA YA UZIMA WA MILELE
"Wala hakuna wokovu katika mwingine, kwa maana hakuna jina lingine chini ya mbingu waliopewa watu tupate kuokolewa nalo." Matendo 4:12
NAMNA YA KUPATA NJIA YAKO KWA MUNGU
1.
Kubali wewe ni mwenye zambi [umemuasi
Mungu].
"Kwa sababu wote wamefanya zambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu." Waroma 3:23
2. Kuja kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.
"Naye [Yesu], kwa sababu hii anaweza kuokoa kabisa wao wanaokuja kwake Mungu kwa njia yake...." &emdash;Waebrania 7:25
3. Tubu zambi zako.
(Kutubu maana yake kujuta sana ku acha zambi.)
"Tubuni basi, mugeuke, ili zambi zenu ziondoshwe...." Matendo 3:19
"Acha uovu, na tenda mema...." Zaburi 37:27
6.
Amini Yesu Kristo.
"...Kama ukikiri kwa kinywa chako ya kuwa Yesu ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimufufua toka wafu, utaokolewa." Waroma 10:9
7. Pokea Yesu Kristo moyoni na maishani mwako.
Unaweza tu kufungua mulango wa moyo wako na kua- lika Yesu kuingia. Yesu akasema: "Tazama, ninasimama kwa mulango, ninapiga hodi; kama mutu akisikia sauti yangu na kufungua mulango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami." Ufunuo 3:20
MWONGOZO WA MAOMBI
Kama haujaomba mbele na unahitaji musaada kwa kuomba, unaweza kufuata maombi haya kama mwongozi:
Bwana Yesu mupenzi, Asante kwa kifo chako musalabani kuondoa zambi zangu. Ninasikitika kwa mambo yote mabaya niliyoyafanya. Tafazali ninakualika kuingia na kukaa moyoni mwangu milele. Ninakuamini kweli sasa kusaficha moyo wangu. Ninakupokea kuwa Bwana na Mwokozi wangu wa pekee. Katika jina la Yesu, Amina.
PAMOJA NA YESU MOYONI MWAKO UNA UZIMA WA MILELE
"...Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu ni katika Mwana wake. Yeye aliye na Mwana ni mwenye uzima...." 1 Yoane 5:11, 12
"...Yeye anayesikia neno langu na kumwamini yeye aliyenituma ...amepita kutoka mauti kuingia uzima."Yoane 5:24
NAMNA YA KUENDELEA KUFWATA YESU
Soma mashairi katika Biblia (Neno la Mungu) siku zote na uyashike moyoni mwako kwa njia ya kujifunza kwa ufahamu mashairi muhimu ambao yamekusaidia. (Mengi ni ndani ya kitabu hiki kidogo.) "Kila andiko limepewa kwa maongozi ya Mungu, na linafaa kwa mafundisho, na kwa kuonya watu juu ya makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa mafundisho katika haki." 2 Timoteo 3:16
YESU ANAKUHITAJI KUSHUHUDIA WENGINE
(nyumbani, chuoni, kanisani, pahaili pote)
Yesu akasema: Kwenda kwa nyumba yako kwa watu wako kuwaambia maneno makubwa gani Bwana aliyofanya juu yako na namna alivyokurehemu. Marko 5:19
HAKIKA YA UWEPO WA MBINGU
Ndani
ya maono ya Yoane katika Ufunuo 21 aliona mbingu mupya na dunia
mupya. Naye atapangusa kila chozi katika macho yao; wala mauti
haitakuwa tena; wala maombolezo, wala kilio, wala uchungu hautakuwa
tena; kwa maana maneno ya kwanza yamekwisha kupita. Na yeye anayeketi
juu ya kiti cha ufalme akasema: Tazama, ninafanya yote kuwa mapya....
Ufunuo 21:4, 5
Yoane aliona vile Muji takatifu, Yerusalem mupya, ukishuka toka kwa Mungu mbinguni. "...Na muji ule ulikuwa wa zahabu safi, mufano wa kioo safi. Na misingi ya ukuta wa muji ilikuwa imepambwa kwa mawe ya bei ya damani ya kila namna ...." Ufunuo 21:18, 19
YESU AMEKWENDA KUTENGENEZA NYUMBA KWA WOTE WANAOMWAMINI
Musifazaike mioyoni mwenu: munaamini Mungu, muniamini mimi vilevile. Katika nyumba ya Baba yangu ni makao mengi; kama sivyo ningaliwaambia ninyi; ninakwenda kuwatengenezea ninyi pahali. Na kama ninakwenda kuwatengenezea ninyi pahali, nitakuja tena, na nitawakaribisha ninyi kwangu; pahali ninapokaa mimi, mukae vilevile. Yoane 14:1-3
YESU ANAKUJA TENA
Kila mutu atafufuka toka wafu. "...Saa itakuja na watu wote walio katika makaburi watasikia sauti yake, nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuko wa uzima, na wale waliofanya mabaya, kwa ufufuko wa hukumu." Yoane 5:28, 29
Wafu katika Kristo watafufuka kwanza.
"Kisha sisi tulio hai, tuliobaki, tutanyanyuliwa pamoja nao katika mawingu, kukutana na Bwana katika hewa, na hivi tutakuwa pamoja na Bwana milele." 1 Watesalonika 4:17
"...Tazameni, ombeni, maana hamujui wakati ule." Marko 13:33
YESU ATAKUJA JE?
"Tazama anakuja na mawingu; na kila jicho litamwona...." Ufunuo 1:7
Angalisho kwa wapinga Kristo na manabii ya uwongo.
"...Wakati mutu atakapowaambia ninyi: Tazama, Kristo ni hapa, ao kule; musiamini. Basi kama wakiwaambia ninyi: Tazama, yeye ni jangwani; musitoke; Tazama, yeye ni katika vyumba vya ndani nyumbani, musisadiki." Matayo 24:23, 26
YESU ATAKUJA UPESI KATIKA MAWINGU YA MBINGU
"Kwa maana kama umeme unavyokuja toka mashariki na unaonekana hata mangaribi; hivi kuja kwa Mwana wa watu kutakavyokuwa vile. ...Na mataifa yote ya dunia...wataoma Mwana wa watu akikuja katika mawingu ya mbingu pamoja na uwezo na utukufu...." Matayo 24:27, 30